ushauri

Fay Pub

Fay Pub
Fay Pub Sinza,We Rock,it is a good place to be cool and usalama wa kutosha!!Fay Pub ipo Sinza kumekucha,nyuma ya Seven Up kama unaelekea shamool Hotel,, kwa maelekezo piga namba 0715 556453

tangaza

Wednesday, September 12, 2012

KALAPINA AFUNGUKA KWAMBA PROF.JAY ANAPOTEA KWENYE RAMANI YA MUZIKI.

Msanii wa hiphop Kalapina wa kikosi cha Mizinga amekubali kutaja majina ya wasanii wa hiphop anaosikiliza muziki wao kwa sasa hapa Tanzania.

Namkariri akisema “Tanzania mimi nasikiliza wasanii wote niangalie vitu wanavyovifanya lakini wasanii wengi hawako real wanafake, sasa hivi nimekua nikiwasikiliza wadogo zangu Lunduno, Nash Mc, Fid Q, Mansu Lee, Rado… mzee mwenzangu Profesa J amepotea sasa hivi, nilikua namsikiliza lakini sasa hivi amepotea”



“Profesa J amefikia hatua anafanya video za dada zetu wako uchi kabisa na ule ni udhalilishaji wa kijinsia kama atabisha si udhalilishaji, achukue video awachukue dada zake na mama zake wadogo awavalishe vichupi na sidiria tutaona kweli yeye ni mmagharibi lakini kama anachukua dada za watu huu ni udhalilishaji wa kijinsia mi napinga mambo kama yale, tusifikie huko sasa hivi huwezi kufanya video kali mpaka uweke wanawake wako uchi Tanzania” – Kalapina

Source;Millard Ayo

No comments:

Post a Comment