ushauri

Fay Pub

Fay Pub
Fay Pub Sinza,We Rock,it is a good place to be cool and usalama wa kutosha!!Fay Pub ipo Sinza kumekucha,nyuma ya Seven Up kama unaelekea shamool Hotel,, kwa maelekezo piga namba 0715 556453

tangaza

Tuesday, April 30, 2013

BIERBER AKUTWA NA MAdAWA YA KULEVYA KATIKA BASI LAKE LA TOUR.


Polisi nchini Sweden wamedai kukuta dawa za kulevya katika basi linalotumiwa na mwanamuziki Justin Bieber anapofanya ziara zake za kimuziki.
Msemaji wa polisi Lars Bystrom amesema kiwango kidogo cha dawa za kulevya na silaha moja vimekutwa katika basi hilo wakati polisi walipolivamia likiwa halina mtu na kuegeshwa katika ukumbi wa Globen mjini Stockholm ambapo mwanamuziki huyo alikuwa akifanya shoo.
Polisi huyo amekata kutaja aina ya dawa zilizokamatwa akisema zimepelekwa maabara kwa uchunguzi.
Hata hivyo hakuna mtu aliyekamatwa.

WALICHOSEMA UVCCM KUHUSU LEMA,BASHE NA UCHAGUZI WA KATA.



BABA MZAZI WA CHRIS BROWN AMTEMA RIHANNA NA KUMKUBALI SPARKS

Gazeti la New York Daily News limefanya Exclusive interview na baba mzazi wa mwimbaji staa Chris Brown na kutoa maoni yake kuhusu mahusiano ya kimapenzi ya mwanae na Rihanna RiRi.


Clinton Brown amesema “sioni maisha marefu kwa Chris Brown kuwa na Rihanna, sijawahi kupendezwa na kurudiana kwao, unajua ni lazima kwenye uhusiano wa kimapenzi uwe na mtu sahihi ambae ni hitaji la kweli na linaloweza kuwa lako kwenye maisha, lakini sio kama hivi”

Clinton amesema hapendi kutumia mifano lakini anadhani watu wameona mahusiano ya mastaa kama Whitney Houston, Michael Jackson, Amy Winehouse na wengine”



Kuhusu mrembo ambae angependa kuona anaolewa na mwanae, Clinton amemtaja Jordin Sparks kwa kusema “nimempenda Jordin, ni msichana mdogo lakini mwenye upeo mkubwa… ana akili na heshima”

Monday, April 29, 2013

MAPENZI

3 top lies from Guy's
_i'm Sorry
_i love You
_i won't hurt you
 


3 top lies from girls
_i'm fine
_i'm not mad at you
_i don't love you
 

CHEATERS MPOOO!!

When A Cheater Says 
" I Won't Cheat On You Again " . 
They Really Mean " I Slipped , 
But Next Time You Won't Catch Me " .


MONEKANO MPYA WA KIM KARDASHIAN AKIWA NA UJAUZITO.



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI TOKA KWA LADY JAYDEE.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Katika mwaka huu 2013, Inatimia miaka 13 tangu nianze kazi ya muziki.
Nashukuru MUNGU tuko pamoja na pia, nashukuru umma wa Tanzania kwa kuendelea ku support muziki wa Tanzania na kunipa nguvu mimi kama msanii.
 
Nashukuru vyombo vyote vya habari vinavyoshiriki kikamilifu kukuza na kulinda sanaa ya Tanzania bila kujali maslahi binafsi.
Tumeandaa sherehe kubwa na nzuri ya miaka 13 ya LADY JAYDEE, katika muziki.
 
Na mdhamini mkuu kwa upande wa media ni East Africa TV.
Sherehe ya miaka 13 ya Lady JayDee katika muziki itaambatana na uzinduzi wa album yangu ya sita inayokwenda kwa jina la NOTHING BUT THE TRUTH ambayo ina jumla ya nyimbo 10.
 
Katika sherehe hizo pia kutakuwa na show ya nyimbo zote bora za JayDee nikishirikiana na baadhi ya wasanii wenzangu hapa nchini.
Sherehe zitafanyika Ijumaa tarehe 31 May 2013.
Nawakaribisha wote tufurahi pamoja
Na Mungu awabariki

LEMA AACHIWA KWA DHAMANA . MJI WALIPUKA KWA SHANGWE.


Sunday, April 28, 2013

PAKUA MZIGO HUU WA UPCOMING ARTIST BY dA NAME OF diga boy FROM BUKOBA BUT NOW ANAPATIKNA ARUSHA THEN MSHAURI KWENYE GAME AFANYE NINI ILI NA YEYE ATUSUE KAMA AKINA NANIIII

All the way from Bukoba muite diga boy 
diga boy himself

Its yo boy Fredy na
diga boy all the way from Bk

phone namba 0754745593
facebook anatumia edger method
ngoma imepikwa na
dj max

studio ni tongue records
click hapa chini uidownload then uniambie mshikaji analack nini ili kwenye game ya bongo now akae poa na atusue kama hao wengine akina Belle na akina Mavoco
click hapa ili kuipakua HAPA!!

MREMBO WA KIBONGO!

 
Unazijua cfa za mrembo wa mjini? 
1.Anatakiwa ajue ku-drive hata kama hana gari 
2.Awe na elimu ya chuo hata kama ni level ya certificate 
3.Awe anajua kuongea english hata kama ni code-switching  
4.Awe anajua kupangilia nguo na via2 hata kama ni za bei rahis na ajue kujipamba 
5.Asijipendekeze kwa mwanaum >:/ hata km anavutia waje wnyw.
6.Ajue kujishugulisha hata kama hana kinachomshugulisha  
7.Ajue hbr za nje na ndani hata kama hazimuhusu
 

SMILE!!

 
Smile is the Best Credit Card.
Bcoz it is Accepted World Wide,
Auto Reload,
Unlimited Usage,
No Payment,
at all makes every1 Happy.
So keep Smiling.

GIRLS KAZI NI KWENU

 
BEFORE SEX*
 
1ST SCENE
JAMAA:"Mbona unajikuna sana kichwani swty?"
DEM:"Beib nywele zinaniwasha kweli."
JAMAA:"Itabidi uende salon(huku anatoa wallet mfukoni)
 

2ND SCENE
JAMAA:"Swity njoo home...nakungoj­a."
DEM:"Acha nichukue bus nakuja."
JAMAA:"Aaa chukua taxi,bus utachelewa."
DEM:"But beib..."
JAMAA:"But ya nini mrembo...we chukua taxi mi nitalipa."
DEM:"Ok beib am on ma way."
 
3RD SCENE
JAMAA:"Hi ma love morning,how was ur nyt?"
DEM:"Morning 2 u darling..it was gr8"

 
4TH SCENE
JAMAA:"Mbona kimya hun hata sms sioni?"
DEM:"Sina airtime."
JAMAA:"Acha nikimbie dukani nakusambazia credit sasa hivi hun."
DEM"Sawah beib am waiting."
 
5TH SCENE
DEM:"Beib am going out 2nyt."
JAMAA:"Aaah usiende bana hao marafiki zako wa kike siwaamini,watak­­ utafutia msela mwengine."
DEM:"Dont worry swty i only love u..mwaah "
 

 
*AFTER SEX*
 
1ST SCENE
JAMAA:"Acha kujikuna kichwa nawe."
DEM:"Jamani beib nywele zinaniwasha."
JAMAA:"Unataraj­­ia nini kama huzisafishi lazima ziwashe."
DEM:"Eeh jamani ishakuwa hivyo hun."
JAMAA:"Si unyoe tu nikupe 20 uende kunyoa?"
 
2ND SCENE
DEM:"Swty uko home nije?"
JAMAA:"Yep panda bus hapo uje..fanya haraka coz nataka kutoka."
DEM:"Lo! haya ma dear nakuja."
 
3RD SCENE
DEM:"U ok beib,yaani toka asubuhi hujanitext."
JAMAA:"Pole nilikuwa busy sana..sina tym ya kutext ovyo ovyo."
 
4TH SCENE
DEM:"Nitumie credit tuchat."
JAMAA:"kwani okoa jahazi ni ya kazi gani,ambia safaricom watakupa."
DEM:"Tobaa...po­­a tu."
 
5TH SCENEDEM:"Beib am going out."
JAMAA:"Najua waenda kutafuta mwengine...nend­­a na usinipigie tena!!";) 

SOMA HII MUHIMU KWAKO.

22 WAYS ON HOW TO KEEP A RELATIONSHIP
 
1. Build trust
2. Be honest
3. Be faithful
4. Be considerate
5. Respect each other
6. Become best friends
7. Be proud of one another
8. Be there for one another
9. Bear each other?s burden
10. Make time for one another


 

11. Communicate to each other
12. Trust and always pray to God
13. Accept each other?s mistakes
14. Appreciate each other?s effort
15. Take time and study each other
16. Love each other unconditionally
17. Refresh your love with surprises
18. Talk about things, both good and bad
19. Know that you won?t always be happy
20. Know that having arguments are normal
21. Forgive and forget each other?s mistakes
22. Leave the past to the past, which include ex`s
 

Thursday, April 18, 2013

KAMA ULIKUA HUJUMJUI MBUNGE ALIETUKANA JANA LIVE BUNGENI NI HUYU HAPA MHESHIMIWA PETER SERUKAMBA.

 Jana kutoka bungeni kimeibuka kioja cha mwaka baada ya wabunge kuja na stail ya matusi bungeni

Mh.Peter Serukamba jana hii amesikika waziwazi bila ya aibu kabisa akitoa tusi mbele ya bunge na hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi yake.

Alisikika akisema hivi "Come-on F.U.*.K Y.O.U."
 
 

KABLA YA KAULI HIYO KUTOKEA ILIANZIA HUKU

Hotuba ya kambi rasmi ya upinzani iliitaka serikali iwachukulie hatua kali wahusika wote wanaohusika na matukio ya utekwaji na uteswaji wa baadhi ya watu,kwa kutolea mifano ya Dr.Ulimboka na Kibanda.katika hotuba hiyo,kambi imeonesha kutoridhika na mwendendo wa utendaji wa idara ya usalama wa taifa.

Aidha hotuba hiyo kuna mahali imemtaja Rwakatare na mwenendo wake kabla ya kukamatwa.
Shida imeanza pale ambapo Mh.Serukamaba aliomba mwongozo wa spika,na kusema kuwa,kuna baadhi ya maswala yaliyomo ktk hotuba hiyo (hasa kuanzia ukurasa wa 1-4) yanazungumzia kesi ya Rwakatare ambayo tayari ipo mahakamani.

Na kwamba kuendelea kusomwa kwa hotuba hiyo ingekuwa ni kuingilia mwenendo wa kesi na kwamba hapo ingekuwa ni kuingilia uhuru wa mahakama.

Katika kutetea hoja zao,wabunge watatu wa kambi ya upinzani(H.Mdee,J.Mnyika na T.Lisu) walisimama na kujaribu kuonesha uhalali wa hoja zao.Wote watatu walijieleza kwa kadiri walivyoona inafaa.

Baada ya hapo ndipo aliposimama Mh.Serukamba na kusisitiza uhalali wa hoja yake.
 
 

Sasa kile kitendo cha yeye kusimama tena,inaonekana kulikuwa na minong'ono upande wa pili(lakini hiyo haikusikika) ndipo alipojikuta akiropoka maneno hayo  hewani tena bungeni "Come-on F.U.C.** Y.O.U."!

Kwa jinsi alivyotukana,aliunganisha haraka na maelezo yake kiasi kwamba Mh.J.Ndugai(aliyekuwa akiongoza) hakumkatisha, akamwacha aendelee.

Baada ya maelezo ya Mh.Serukamba,naibu spika(mwenyekiti) alitoa kauli yake rasmi.

Ndugai amesema kuwa mgogoro huu una mtazamo wa kikanuni,kwa hiyo ameagiza kamati ya kanuni ya bunge ikutane mara moja kujadili swala hilo kisha itoe ushauri kwa kiti cha spika jinsi gani ya kshughulikia mambo hayo yanayoonekana yana utata.

SOMA HAPA MAKALA NA MAHOJIANO YA MWISHO YA BI KIDUDE KABLA YA UMAUTI KUMKUTA.

FATMA binti Baraka, maarufu kwa jina la Bi Kidude, ni miongoni mwa wasanii wanawake wachache ambao ni magwiji wa muziki wa taarabu nchini, ambaye kwa siku ya leo ataibeba manowari yetu ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka ifikapo Machi 8.
Bibi huyu mwenye sauti nzito na inayopenya vyema masikioni mara anapoimba, ni mzaliwa wa Zanzibar lakini asili ya kabila lake ni Mmanyema kutoka Mkoa wa Kigoma, magharibi mwa nchi.


Licha ya kuwa na umri mkubwa (113) , sauti ya Bi Kidude bado ni nzuri na yenye kuvuta hisia, hasa kwa mpenzi wa miondoko ya muziki wa mwambao.
Bi Kidude katika nyimbo zake nyingi amekuwa akiwavutia wengi kutokana na nyimbo zake kubeba ujumbe wa mahaba kama alivyoimba kwenye wimbo wake ’Ya Laiti napenda pasi kifani’ na wakati mwingine mafumbo kwa lugha ya Kiswahili yenye lengo la kufikisha ujumbe kwa watu maalumu kama alivyoimba katika wimbo wake wa ’Muhogo wa Jang’ombe’.


Hadi hapo utaona kwamba mtu mzima huyu anapaswa kupewa heshima katika siku kama hii, hasa kwa kuzingatia kwamba ni Siku ya Wanawake Duniani.
Historia na asili ya jina Kidude Fatma Baraka kwa kauli yake, anasema amezaliwa miaka 113 iliyopita huko Zanzibar ambako baba yake mzazi alilowea akitokea Kigoma (enzi za utumwa), hivyo kabila lake ni Mmanyema, tena mwenyewe anajiita ni Mmanyema asilia.
Ingawa hafahamu kijiji halisi alichozaliwa baba yake, Bi kidude anasema babu yake upande wa mama alikuwa Mngindo, wenyeji wa Kilwa.
“Mimi asili yangu ni Mmanyema wa Kigoma, baba yangu na mama yangu alikuwa Mngindo, lakini baba yangu alilowea Zanzibar, ndiyo nasisi tukazaliwa huko mpaka sasa naishi Zanzibar, lakini mie Mmanyema,” anasema Bi kidude alipozungumza na Tanzania Daima hivi karibuni.


Anasema jina la Kidude alipewa na mjomba wake wakati alipozaliwa kwa sababu alikuwa na umbile dogo. “Nimezaliwa miezi saba... njiti, nililazwa kitandani, nilikuwa mdogo, mtu hawezi kujua kama kuna kitu kimelazwa.
“Kuna mjomba wangu akaja akakaa nilipolazwa mimi, akaambiwa angalia usimkalie mtoto, akasema mtoto gani, ni kidude tu hiki, basi ndo tangu siku hiyo jina limenieleleza.
Mkongwe huyu wa taarabu nchini, ambaye kwa miaka ya hivi karibuni amejizolea umaarufu kupitia tasnia hiyo, anasema katika maisha yake hajapata kuwa na mtoto, ingawa ameweka bayana kwamba aliwahi kuolewa mara mbili.
Kwa muonekano ni kikongwe mwenye nguvu zake, anasema katika umri alionao, amepitia misukosuko ya aina tofauti za maisha. Kifupi, safari yake kimaisha ni ndefu.
Anafafanua kwamba ndoa yake ya kwanza alifunga na Ramadhani Ibrahimu, na wa pili aliitwa Juma Kombo.


“Nimeolewa vyuo viwili, cha kwanza nikaachika, nimewahi kumfumania mume wangu (nadhani anamaanisha huyo wa pili), nikampiga kwa mikia ya taa nikamwacha anachuruzika damu, nikaenda zangu na mpaka leo sijaolewa na wala sina haja ya kuwa na mume,” anasema.
“Sijisifu, ila miye mpaka kesho ukiniudhi wallahi sitafuti mtu... nitawatuma watu wakuite, ukifika mie nimeandaa fimbo yangu, nikikuchapa nayo, ikimpata mtu anasimama kama anatafuta pesa,” anasema Bi kidude na kuongeza utani, jambo linalokulazimu kuendelea kumsikiliza bila kuchoka.


Anaendelea kuwausia hususan wasichana walio katika umri wa kuolewa kwamba wanaume wa sasa hivi si wema wengi wanapenda kumkuta mwanamke ana kila kitu. “Hakuna wanaume sasa hivi, hao walikuwepo zamani, siyo leo... leo mwanaume anakufuata, umlishe, umfanyie kila kitu, waapiii! Wanaume enzi hizo,” anasisitiza Bi kidude.
Maisha yake na uimbaji Mkongwe huyu wa taarabu na muziki wa mwambao nchini anainadi siri yake katika fani kuwa ni kipaji. Katika hilo Bi Kidude anasema ameanza kuimba akiwa binti wa miaka 10, alipokuwa akitoroka kwao na kwenda nyumbani kwa marehemu Mtumwa binti Saadi, maarufu Siti binti Saad.
Kadhalika, anatanabaisha kwamba mafanikio kwa mwanamuziki bora ni yule anayetumia kichwa na dhati ya moyo wake kwenye kuimba. Anasema kubana au kuibadili sauti wakati wa kuimba si sahihi, inamtoa mwimbaji kwenye uhalisia wake.


“Mie naimba kwa kutumia kichwa, si kifua au kubana pua aaa! Sifanyi kama hao wanaojiita waimba taarabu wa siku hizi, kwanza siku hizi hakuna taarabu. Mimi nina uwezo wa kuimba bila kutumia karatasi... kwani bendi ya polisi! (kicheko kwa wanaomsikiliza).
“Enzi zetu taarabu ulikuwa mtu ukiisikiliza ufanye kazi kupata maana yake kutaka kulinda matusi na kila mmoja anaweza kuisikiliza popote. Kwanza watu walikuwa wanaanza kuimba saa nane za usiku, ikifika saa 11 unafungwa muziki. Mie nashangaa siku hizi taarabu inaanza saa mbili.



“Taarabu ya zamani mtu ulikuwa ukitisa kichwa taratibu, wanawake tulikuwa tunavaa kwa heshima, si siku hizi watu mnakatika mabuno (viuno), wanawake wanakwenda bila heshima, au kwa vile kuna matako ya Kichina?” anahoji mwanamuziki huyo huku akitoa pakiti yake ya sigara aina ya Embassy na kuvuta.


Kuhusu sigara na uimbaji, Bi kidude hakubaliani na dhana kwamba inamaliza sauti, badala yake anashuhudia kwamba ameanza kuvuta akiwa kijana lakini sauti yake haina mabadiliko.
“Nimevuta sigara mie hujazaliwa na mpaka sasa navuta sijapata TB wala ugonjwa wa mapafu, leo unaniambia mbaya! Mbona sijafa?” anahoji mkongwe huyo na kueleza kwamba alianza kuvuta sigara aina ya Seven Seven, Mkasi, Simba, Kulindondo, Gundufleki na sasa Embassy ambapo ana uwezo wa kumaliza pakiti moja kwa siku tatu.
Mbali ya kuimba, pia Bi kidude ana uwezo wa kupiga ngoma, ikiwa ni baada ya kujifunza kwenye majahazi wakati akiwa na umri mdogo alipokuwa akitoroka kwenda madrasa (chuo cha elimu ya Kiislamu).


“Nilikuwa nakimbia nyumbani, naaga naenda chuo lakini sifiki, nazuga kwa kubeba juzuu yangu kwapani lakini siendi huko, bali nakwenda kwenye majahazi kufundishwa kupiga ngoma na tumba,” anasisitiza.
Oktoba mwaka 2005 alipata Tuzo ya heshima ya msanii mwenye mafanikio makubwa iliyotolewa nchini Uingereza (tuzo ya WOMAX).
Aliyebaini kipaji chake Bi Kidude, anapasua ukweli kwamba mtu wa kwanza kuthamini kazi zake na kumtafuta hadi kufika alipo alikuwa Rais mstaafu wa Tanzania wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi. 


Anasema alipokuwa Rais wa Zanzibar, aliwaomba watu wamtafute Bi Kidude ili apate kumwimbia nyimbo za Siti, kwa kuwa hakuna aliyeweza kuziba pengo japo kidogo la Siti binti Saad.
“Ali Mwinyi alikuwa akitafuta nyimbo za Siti binti Saad. Akatumwa Vuai na Khadija Baramia ambao siku nyingi hatujaonana.
“Walipotokea wakaniambia natafutwa na Ali Hassan Mwinyi, mie nikashangaa, kwa sababu nyumba zetu zilikuwa zikitizamana milango, nikaona bora niende... nikapelekwa Bwawani nikatengenezewa chumba kama kuku.


“Teena! Nikawa namwimbia Mwinyi kule Bwawani akija anaburudika... huko nikakutana na Mariam Hamdani (dada wa aliyekuwa Waziri wa Fedha, Zakhia Hamdani Meghji) alikuwa anakuja kunipiga picha anapeleka Ujerumani miye Bi Kidude sijui,” anasema.
Aidha, anafahamisha kwamba alipelekwa kwa mara ya kwanza nchini Ujerumani na Mariam Hamdani, aliyemtambulisha kwa watu mbalimbali ambapo aliweza kusimama kwenye majukwaa na kutumbuiza.


Kama hiyo haitoshi, Bi kidude anaongeza kwa kusema Mariam alimpeleka hadi kwa Malkia Elizabeth II nchini Uingereza. “Yeye ndiye alinipeleka Ulaya, sikujua Kiingereza, nikawa na mlinzi, miye nimefika hadi kwa Malkia Mtukufu Lizabet (Elizabeth)... akawa ananisalimia Shikamoo mama Kidude.
“Nimepewa cheo na Mtukufu Lizabet. Nilipofika anafunua vitabu naona sura yangu nikawa nashangaa, alinipa kidani cha dhahabu nikaamua kukiuza kulekule Uingereza, maana ningekuja nacho huku wangeniua,” anasema.


Katika hilo, Bi kidude anasema alipofika kwenye kasri la malkia alikutana na askari waliofanana na sanamu, wamevalia viatu vya chuma huku akieleza kwamba hajawahi kuliona kochi kama aliloliona huko.
“Wakati natoka kwa Mtukufu Lizabet nilijikojolea ndani ya gari kwa hofu mambo niliyoyaona makubwa,” anasema Bi Kidude ambaye ni binamu wa aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Salmin Amour.


Akiwa nje ya Tanzania, mkongwe huyo anaeleza anavyothaminiwa huku akisisitiza kwamba Mkurugenzi wa Nyumba ya Vipaji Tanzania (THT), Ruge Mutahaba, pia alimsaidia na kumfikisha alipo.
“Mimi, Ruge miye sikumjua huku, kanikuta napiga ngoma kwa Shakira, kanipenda akanichukua kaenda kunikodia hoteli alipojua naimba ndo akanikaribisha ofisini kwake, tunaongea ananihoji, kisha ananipa pesa anaondoka, mie nabaki hotelini tena.
“Siwi na shida miye, nakwenda ofisini kwa Ruge, simuombi mwenyewe ananigawia pesa, ananiuliza upo au haupo, namwambia narudi Unguja na yeye akija Unguja lazima afike nyumbani kwangu, anachukua alichonacho ananigawia, simuombi aah! Ananitumikia yeye. Hii ni mara ya pili anakuja kunichukua kwa ajili ya tamasha,” anasisitiza huku akimwomba Mungu ambariki mkurugenzi huyo.


Miongoni mwa nyimbo zinazompa umaarufu Bi kidude hadi sasa ni Muhogo wa Jang’ombe, Yalaiti, Kijiti, Arebaba na Machozi, Machozi ya huba na nyinginezo.
Anavyoijua Dar es Salaam Bi kidude anasema anaifahamu vilivyo Dar es Salaam kwa kuwa amefika hapa enzi za utawala wa Mwarabu wakati wazawa wakitoa kodi ya kichwa.
“Nchii hii kaitengeneza John Rupia miye niko hapa, mama Haambiliki alikuwa anafanya vichekesho, nimemlea miye, mama mzazi wa mwanamuziki Shakira nimemlea miye. Hao kina Mzee Yusuf nimewalea wazazi wao.
“Nimekuja hapa binti sijaolewa, nimekuja kwa madhumuni ya kuimba taarabu, nilifikia Bagamoyo, Rais Jakaya Kikwete, kazaliwa mikononi mwangu mie, nilikuwa naishi kwa Sheikh Ramia.


“Nimewahi kuishi Ajipshini (Egyptian) kwa miaka tisa,” anasisitiza gwiji huyo wa miondoko ya taarabu ambaye hivi karibuni alikonga nafsi ya Rais Kikwete na Watanzania waliohudhuria uzinduzi wa kampeni ya Mradi wa Malaria iliyokwenda kwa jina la ’Zinduka.’

NAIBU SPIKA AWAPA WABUNGE WATANO AdHABU YA KUTOHUdHURIA VIKAO VYA BUNGE WABUNGE KWA SIKU TANO.

Naibu Spika wa Bunge JOB NDUGAI amemtoa nje ya Bunge kwa muda wa siku tano Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni TUNDU LISSU kwa madai ya utovu wa nidhamu na kuanzisha majibizano bungeni kitendo kinachokiuka kanuni za bunge.


 Wengine ambao wamepewa adhabu hiyo ya kutohudhuria vikao vya bunge kwa siku tano ni Mbunge wa Mbeya Mjini JOSEPH MBILINYI, Mbunge wa Arusha Mjini GODBLES LEMA, Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji PETER MSIGWA, Mbunge wa Nyamagana EZEKIA WENJE na Mbunge wa Ilemela HIGHNES KIWIA ambao walikuwa wakiwazuia askari wa bunge kumtoa nje LISSU.
Namkariri Naibu Spika akiongea  nje ya bunge akisema “nimemuonya zaidi ya mara kumi kwa jioni ya leo peke yake kwamba demokrasia ya kibunge ni ya kuwapa watu wengine nao nafasi ya kusikika, kila anaesimama anakatishwa yeye kasimama dakika zake zote amekatizwa na kina nani? kinachokosekana kwenye bunge hili ni uvumilivu wa kumsikiliza mwingine, watu wanapenda kumshambulia mwingine lakini hawako tayari kusikiliza wengine wakiwajibu, tunalaumiwa na kila mtu….. hata hatua nilizozichukua ni hatua ndogo tu”
Kabla ya uamuzi wa kutolewa nje ya Viwanja vya bunge haujatolewa, Mbunge wa Iramba Magharibi MWIGULU NCHEMBA ndiye aliyekuwa akichangia Bajeti ya Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma ambapo namkariri hapa akisema “mimi ni ninachokumbuka labda watu wengine kumbukumbu sijua wanakua na hangover gani, kitu ninachokitambua kwamba Rais amekua mtu wa kwanza kukemea jambo la udini, kuna mgombea wa chama kimojawapo alikua anakwenda anaongea na baadhi ya Viongozi wa kidini kama ndio viongozi na mikutano ya ndani ya chama chake, hili linakubalika wapi? wakari CCM inatumia mabalozi, wenyeviti wa tawi…..”
Mbunge wa Longido LEKULE LAIZER ni kama ametabiri kutokea kwa jambo hilo kabla kwani wakati anachangia amepinga vitendo vya vurugu bungeni hali iliyopelekea kuwakumbuka wabunge wa zamani.





CreDits; MillarD Ayo



MISTARI HII IMEMPONZA ROOOZEY KUKOSA SHAVU LA REEBOK

Hiki ndio kijipande cha verse kilichomponza Rick Ross;

I die over these Reeboks, you ain't even know it
Put Molly all in her champagne, she ain’t even know it
I took her home and I enjoyed that, she ain't even know it

Got a hundred acres I live on, you ain't even know it
Got a hundred rounds in this AR...

Hii ndio ngoma nzima ya Rocco 'U. O. E. N. O' ft Rick Ross, Rocco ni msanii mpya wa lebo ya MMG ambaye inaweza ikasemwa kuwa ngoma yake Rick Ross huku ndani na kumsababishia balaa.

Wednesday, April 17, 2013

BAAdA YA dIAMONd KUSAMBAZA VOICE NOTE YA WEMA AKIMUOMBA MSAMAHAA WARUdIANE HIKI NdICHO WEMA ALICHOPOST INSTAGRAM.


BREAKING NEEEEWZZZZ!!!!! BI KIDUDE HATUKO NAE TENA DUNIANI.

MSANII WA MUZIKI WA TAARABU NCHINI TANZANIA KUTOKA VISIWANI ZANZIBAR FATUMA BINT BARAKA MAARUFU KAMA BIBI KIDUDE AMEFARIKI DUNIA LEO HUKO VISIWANI ZANZIBAR. NA KWA KUMKUMBUKA TU AMESHA WAHI KUFANYA KAZI NYINGI IKIWEMO MHONGO WA JANG'OMBE, KIJITI, ALAMINADURA, YA LAITI, AHMADA NA NYINGINE NYINGI.





MUNGU NA AMPUMZISHE MAHALA PEMA PEPONI AMINA.
NA KWA HABARI ZAIDI FUATILIA VYOMBO VYA HABARI.