ushauri

Fay Pub

Fay Pub
Fay Pub Sinza,We Rock,it is a good place to be cool and usalama wa kutosha!!Fay Pub ipo Sinza kumekucha,nyuma ya Seven Up kama unaelekea shamool Hotel,, kwa maelekezo piga namba 0715 556453

tangaza

Wednesday, April 3, 2013

SHIRIKA LA NYUMBA LATOA TAMKO JUU YA GHOROFA LILILOPOROMOKA.

Shirika la nyumba la Taifa NHC limekiri kwamba ndio mmiliki wa kiwanja kilichokua kimejengwa jengo la gorofa 16 ambalo liliporomoka siku kadhaa zilizopita Dar es salaam na kusababisha vifo vya watu 36 na kujeruhi 18.
Mkurugenzi Mkuu Nehemia Mchechu amesema kwa kawaida shirika la nyumba limekua likiingia ubia na watu binafsi wenye uwezo wa kujenga nyumba kama hizo ambapo liliingia ubia na kampuni ya ujenzi ya RAZA na kusaini mkataba wa kujenga jengo lenye gorofa 10 tu kwenye eneo hilo ingawa baadae kampuni hiyo iliomba kubadili mkataba ili wajenge gorofa 16.
Kuhusu umiliki kwa asilimia 25 kwenye jengo lililoporomoka, Mchechu amesema kwa ubia uliokuwepo walipaswa kupewa asilimia hizo baada ya ujenzi kukamilika na asilimia nyingine 25 wangepewa miaka kumi baadae kulingana na mkataba na hawakupaswa kuhusika kwenye gharama zozote wala taratibu za ujenzi.
.
.
Namkariri akisema “february 15 2011 ndio walituandikia kwamba wanakusudia kuongeza gorofa zifike 16 na kwamba wanawasiliana na Mamlaka husika kwa ajili ya kupata vibali hivyo na wakifanikiwa wangeomba kuongezewa muda wa kumaliza mradi na pia baada ya kupata kibali wangetutaarifu kwa ajili ya kufanya marekebisho ya mkataba”
Kwenye line nyingine, NHC imeunda timu kwa ajili ya kufanya ukaguzi katika miradi yake yote ya ujenzi wa ubia ili kujihakikishia usalama wa majengo husika.

Source; Millard Ayo

No comments:

Post a Comment