ushauri

Fay Pub

Fay Pub
Fay Pub Sinza,We Rock,it is a good place to be cool and usalama wa kutosha!!Fay Pub ipo Sinza kumekucha,nyuma ya Seven Up kama unaelekea shamool Hotel,, kwa maelekezo piga namba 0715 556453

tangaza

Thursday, April 18, 2013

KAMA ULIKUA HUJUMJUI MBUNGE ALIETUKANA JANA LIVE BUNGENI NI HUYU HAPA MHESHIMIWA PETER SERUKAMBA.

 Jana kutoka bungeni kimeibuka kioja cha mwaka baada ya wabunge kuja na stail ya matusi bungeni

Mh.Peter Serukamba jana hii amesikika waziwazi bila ya aibu kabisa akitoa tusi mbele ya bunge na hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi yake.

Alisikika akisema hivi "Come-on F.U.*.K Y.O.U."
 
 

KABLA YA KAULI HIYO KUTOKEA ILIANZIA HUKU

Hotuba ya kambi rasmi ya upinzani iliitaka serikali iwachukulie hatua kali wahusika wote wanaohusika na matukio ya utekwaji na uteswaji wa baadhi ya watu,kwa kutolea mifano ya Dr.Ulimboka na Kibanda.katika hotuba hiyo,kambi imeonesha kutoridhika na mwendendo wa utendaji wa idara ya usalama wa taifa.

Aidha hotuba hiyo kuna mahali imemtaja Rwakatare na mwenendo wake kabla ya kukamatwa.
Shida imeanza pale ambapo Mh.Serukamaba aliomba mwongozo wa spika,na kusema kuwa,kuna baadhi ya maswala yaliyomo ktk hotuba hiyo (hasa kuanzia ukurasa wa 1-4) yanazungumzia kesi ya Rwakatare ambayo tayari ipo mahakamani.

Na kwamba kuendelea kusomwa kwa hotuba hiyo ingekuwa ni kuingilia mwenendo wa kesi na kwamba hapo ingekuwa ni kuingilia uhuru wa mahakama.

Katika kutetea hoja zao,wabunge watatu wa kambi ya upinzani(H.Mdee,J.Mnyika na T.Lisu) walisimama na kujaribu kuonesha uhalali wa hoja zao.Wote watatu walijieleza kwa kadiri walivyoona inafaa.

Baada ya hapo ndipo aliposimama Mh.Serukamba na kusisitiza uhalali wa hoja yake.
 
 

Sasa kile kitendo cha yeye kusimama tena,inaonekana kulikuwa na minong'ono upande wa pili(lakini hiyo haikusikika) ndipo alipojikuta akiropoka maneno hayo  hewani tena bungeni "Come-on F.U.C.** Y.O.U."!

Kwa jinsi alivyotukana,aliunganisha haraka na maelezo yake kiasi kwamba Mh.J.Ndugai(aliyekuwa akiongoza) hakumkatisha, akamwacha aendelee.

Baada ya maelezo ya Mh.Serukamba,naibu spika(mwenyekiti) alitoa kauli yake rasmi.

Ndugai amesema kuwa mgogoro huu una mtazamo wa kikanuni,kwa hiyo ameagiza kamati ya kanuni ya bunge ikutane mara moja kujadili swala hilo kisha itoe ushauri kwa kiti cha spika jinsi gani ya kshughulikia mambo hayo yanayoonekana yana utata.

No comments:

Post a Comment