ushauri

Fay Pub

Fay Pub
Fay Pub Sinza,We Rock,it is a good place to be cool and usalama wa kutosha!!Fay Pub ipo Sinza kumekucha,nyuma ya Seven Up kama unaelekea shamool Hotel,, kwa maelekezo piga namba 0715 556453

tangaza

Wednesday, August 29, 2012

CHADEMA YACHANGIA WAFIWA MORO.

KATIBU mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Dk. Wilbroad, Slaa jana
 alilazimika kuendesha shughuli ya kuomba msaada wa fedha kutoka kwa watu waliofurika kwenye mkutano wa chama hicho mjini Morogoro ili kuwachangia wafiwa na walioathirika na vurugu zilizoanzishwa na polisi dhidi ya wafuasi wa chama hicho.
Akifafanua, alisema zitatumika kuwasaidia majeruhi wawili waliopigwa risasi na polisi jana ambao wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro.

Pia fedha hizo zitapekwa kwa familia ya marehemu Ally Zolla anayesemekana aliuawa kwa kupigwa risasi na polisi wakati wa vurugu hizo.

Mmiongoni mwa watu waliozunguka na bakuli hilo ni pamoja na Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika.

Fedha hizo hazikufahamika idadi yake hadi mwandishi wetu anaondoka kwenye viwanja hivyo majira ya saa moja usiku.


Source;Mateja  

No comments:

Post a Comment