ushauri

Fay Pub

Fay Pub
Fay Pub Sinza,We Rock,it is a good place to be cool and usalama wa kutosha!!Fay Pub ipo Sinza kumekucha,nyuma ya Seven Up kama unaelekea shamool Hotel,, kwa maelekezo piga namba 0715 556453

tangaza

Tuesday, September 4, 2012

MISS TANZANIA K-LYNN KUWA MAMA SOON.


YULE MISS TANZANIA ASIYECHUJA UZURI WAKE AMEAMUA KUFATA NYAYO ZA MASTAA KIBAO WA MBELE WANAOPATA WATOTO WAKIWA NJE YA NDOA... KLYINN AMBAYE ALIAMUA KUACHANA NA MUZIKI NA KUINGIA KATIKA MAHUSIANO AMBAYO YAMEDUMU KWA MUDA MREFU NA YULE JAMAA.. SI UNAMJUA? DONT ASK ME ANYTHING... MLIOKUWA MKIPREDICT HAWAWEZI KUFIKA MBALI KATIKA MAHUSIANO YAO SASA MMEUMBUKA AS KLYINN AMEHAMA NCHI KWA MUDA ILI KULEA MIMBA YAKE NA MENGINE YATAFUATA BAADA YA MTOTO KUZALIWA...

LYRICS ZA NYIMBO YA I`M COMING HOME YA MORGAN HERITAGE.

[Intro:]
Oooh yey yea yeey
Ooooooh yeee
I'm coming home baby just hold on
Yeeah

[Verse 1:]
Oooh yey yeah yeeey
Ooh yeah
I'm coming home (yeah)
There was a time when all I wanted to do
Was the only things that mattered to me (yeeah)
But when a man and a woman builds their home
A man's gotta do what his family needs him to do

[Chorus:]
When I come home everything should be alright
So mammy hold on everything will be just fine
So when I'm coming everything should be alright
So baby hold on everything will be just fine

[Verse 2:]
Sad I know you I know you miss the day
And I know the children too
So many times I'm not far away
It's not a few that carry me through the day
It's not easy for a man to live this way
But I do that why I pray

[Chorus:]
When I come home everything should be alright
So mammy hold on everything will be just fine
So when I'm coming everything should be alright
So baby hold on everything will be just fine

[Bridge:]
Hooold on mmmmmm...
Hooold on
You've got to hoooold on
You just tell her hooold on
Eeeh

[Chorus:]
When I come home everything should be alright
So mammy hold on everything will be just fine
So when I'm coming everything should be alright
So baby hold on everything will be just fine

LAWS OF HANDLING A WOMAN.

1) Never take a woman for granted or neglect her. The moment you do, she’ll start scanning the field and you won’t know it.

2) Do not cheat on her, or cheat her. A woman’s revenge could be emotionally lethal.


3)Do not boss her around, push her to do anything she doesn’t want to do, or force her to give you ANYTHING.


4) Do not expect her to wait on you hand and foot. She will take your foot and put it in your hand.


5) Be appreciative for all she does for you and show her appreciation for being in YOUR life. When you start acting like she should be happy she is in YOUR life, she will go out to prove you otherwise.


6) Never lay a hand on her, unless it is to caress her.

WANANCHI WALAANI MAUWAJI YA MWANDISHI WA HABARI IRINGA.

CHAMA cha waandishi wa habari mkoa wa Dodoma (CPC) wamelaani vurugu zilizotokea jana mkoani Iringa na kusababisha kifo cha mwandishi wa habari wa kituo cha utangazaji cha Chanel Ten Daud Mwangosi.
Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa chama hicho Habel Chidawali alipokuwa akitoa tamko hilo mbele ya waandishi wa habari mkoani hapa. Chidawali amesema kuwa kamwe chama hicho hakikubaliani na nguvu kubwa iliyotumiwa na jeshi la polisi kwa ajili ya kumwaga damu ya mwandishi huyo ambaye hakuwa na hatia na kamwe jeshi la polisi haliwezi kujitetea kwa kudai kifo cha mwandishi huyo ni bahati mbaya.
Amesema kuwa jeshi la polisi limekuwa likionyesha wazi wazi kuwa linatumia nguvu,ubabe na matumizi mabovu ya silaha za moto ambayo hayajaweza kusaidia siku zote na badala yake kinachoachwa ni maumivu na vilio kwa wananchi.
Katibu huyo amesema kama jeshi la polisi linatuliza ghasia hakuna siku hata moja haijatokea wakamuua kiongozi yoyote wa siasa ambao ni vinara wa mikutano mbalimbali.
Kwa upande wao wananchi mbalimbali mkoani hapa wamekemea nguvu kubwa inayotumika na Polisi katika vurugu mbalimbali zinazotokea.
Wamesema tabia ya jeshi la polisi kutumia nguvu na silaha za moto ambazo zinasababisha vifo vya watu wasiokuwa na hatia.
Catheline Muhinte, amesema kuwa tukio lililofanywa na jeshi la polisi la kumuua mwandishi wa habari linaonyesha dhairi kuwa kwa sasa jeshi hilo linafanya kazi kwa kukiuka maadili ya malengo yao.
Amesema katika mwonekano wa picha ambazo zinaonekana katika vyombo mbalimbali vya habari inaonyesha dhairi kuwa polisi walihusika moja kwa moja na kifo cha mwandishi huyo.


MAY HIS SOUL REST IN PEACE. amen

Source;Mteja20

MICHAEL ROSS AKIRI KUWEPO KWA NDUMBA KWENYE MUZIKI WA AFRIKA MASHARIKI.

Kuna kipindi wimbi la stori za wasanii Tanzania kutumia uchawi lilipita sana bongo mpaka wasanii wakubwa wakajitokeza kukemea.
Sasa kama ulidhani Tanzania ndio inaweza kuwa nchi pekee afrika Mashariki wasanii wake kutumia juju, utakua umepotea…
Michael Ross anashare experience yake na sisi, akiamini kwamba uchawi kwenye muziki wa Uganda upo pia na watu wanautumia, lakini haamini kama uchawi unaweza kumsaidia.
Kwa miaka yote tisa anasema amefanya muziki na ametengeneza mkwanja na ametengeneza hits bila kujaribu kutumia uchawi, ndio maana haoni umuhimu wa kutumia uchawi ambapo kwenye line ya mwisho, mkali huyu kutoka 256 amesema hata kama msanii atatumia juju nyumbani kwao halitoweza kumsaidia kimataifa.

Monday, September 3, 2012

MWALIMU AACHISHWA KAZI KWA TUHUMA ZA USHOGA.

Uongozi wa Shule ya Sekondari ya Majengo, Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi umeridhia kuacha kazi kwa mwalimu wa kiume wa shule hiyo anayedaiwa kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja.
Kufuatia hatua hiyo, Bodi ya shule imemlipa mwalimu huyo Endrew Katto, Sh. 2,409,924 kama kiinua mgongo baada ya kuitumikia shule hiyo kwa miaka sita.
Mwalimu Katto aliajiriwa katika shule hiyo Februari Mosi, 2006 hadi Februari Mosi mwaka huu, alipoamua kuandika barua hiyo na kumfungulia kesi Mkuu wa shule hiyo, Bruda Peter Lyimo, kwa madai ya kumtukana kwa maandishi katika kituo kikuu cha polisi Mjini Moshi na kufungua jalada Na. MOS/RB/11709/2012
Alipotakiwa na NIPASHE kueleza sababu za kuandikiwa barua hiyo alisema hawezi kuzungumzia kwa undani kwa kuwa alishamuelekeza wakili wake kuchukua hatua za kisheria
Aidha, mwalimu huyo amewasilisha barua ya kutaka aombwe radhi na kulipwa fidia ya Sh milioni 800 kupitia wakili wake Kipoko & Advocate, akidai kuwa Bodi ya shule imemdhalilisha na kuchafulia jalada la taaluma yake hali inayomsababishia asiajiriwe sehemu yoyote.
Hata hivyo, wakili huyo aliiambia NIPASHE kwa njia ya simu kuwa endapo watamuomba radhi mteja wake na kumlipa gharama na kuridhika hawataenda mahakamani
Kwa mujibu wa barua ya Mkuu wa shule hiyo, Bruda Peter Lyimo ya 18/04/2012 yenye kumbukumbu Na. MSS/PP/AK/189/30 imeeleza kuwa uongozi wa shule umeridhia mwalimu huyo kuacha kazi baada ya kubainika kuwa alikuwa akijihusisha na masuala ya kujamiiana kinyume cha maumbile.
“The school administration received your letter dated 12.04.2012 in which you clearly stated that you will not keep on working at this shool as a teacher after a homosexual scandal was revealed on you” (Utawala wa shule umepokea barua yako ya tarehe 12. 04. 2012 ambayo umeeleza wazi kuwa huwezi kufanyakazi katika shule hii kama mwalimu baada ya kubainika kwa kashfa dhidi yako ya kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja),”
ilisomeka sehemu ya barua hiyo ikimaanisha kuwa kuacha kazi kwa mwalimu huyo kulitokana na kubainika kushiriki suala la ushoga.
Akizungumza na NIPASHE ofisini kwake, Bruda Lyimo alikiri kuandika barua hiyo kwa maelezo kuwa aliiandika akiwa makini kwa kuwa ushahidi upo nakuongeza kuwa Majengo Sekondari ni shule inayoheshimika nchini kwa elimu na malezi bora kwa hiyo sio busara kuendelea kuwa na mwalimu aliyekiri kuwa ni shoga.
Habari zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na Mkurugenzi wa Elimu Jimbo Katoliki la Moshi, Padre Wiliamu Ruaichi, zimeeleza kuwa uongozi wa kanisa hilo bado unatafakari hatua iliyochukuliwa na bodi.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

NAMNA HII ELIMU TANZANIA ITABOREKA.

WAKUU wa shule za sekondari nchini wametakiwa kuacha tabia ya kusajili wanafunzi ambao hawajapata nafasi ya kuchaguliwa kujiunga na elimu ya sekondari, kwa kigezo cha kuziba nafasi ya wale waliochaguliwa na kushindwa kuripoti kwa muda mwafaka.
Badala yake wafuate taratibu na kanuni za Wizara ya Elimu  na Mafunzo ya Ufundi katika kusaili wanafunzi.
Viongozi hao waliopewa dhamana ya kusimamia taratibu za kuhakiki wanafunzi wanaojiunga na elimu hiyo, walipewa onyo hilo juzi mjini Kibaha, katika mkutano wa wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania.
Onyo hilo lilitolewa na Mwakilishi wa Mkaguzi Mkuu wa Shule za Sekondari katika Kanda ya Mashariki, Paulo Moshi, ambaye alisema vitendo hivyo vinapingana na sheria za nchi.
Alisema kuwa kitendo cha baadhi ya wakuu wa shule za sekondari kuwasajili kinyemela wanafunzi ambao hawakuchaguliwa, kinarudisha nyuma maendeleo ya elimu.
Alisema hiyo inatokana na ukweli kwamba baadhi ya wanafunzi hao wanakuwa wanaingia katika shule za sekondari, huku wakiwa hawana sifa inayostahiki.
“Napenda kuwasihi juu ya hili kuwa hiki ni kitendo ambacho kinarudisha nyuma maendeleo ya nchi hasa katika nyanja ya elimu, naomba tujirekebishe kama kutakuwa na wanafunzi wanaoshindwa kuripoti kwa muda mwafaka kwa sababu mbalimbali, basi tutumie kanuni zetu zilizowekwa na Wizara ya Elimu,”alisema Moshi.

Alisema katika kuwaingiza wanafunzi wasiokuwa na sifa kunasababisha matokeo mabaya  ya mitihani.

Source;Natafutashule.com